Masomo katika umuhimu wa Tawhiidi Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah

1- Kitabu hiki kinazungumzia masomo katika umuhimu wa Tawhiid kimezungumzia umuhimu wa elimu na mambo manne ambaoyo niwajibu kwakila muislam kuyajua, pia amezungumzia subra na vigawanyo vyake.

2- Risala ya tatu, mambo matatu ambayo nilazima muislam ajifundishe, pia kimeleza sababu ya kuumbwa mwanadamu, na lengo la kutumwa mitume, na adhabu tatu za watu wa firauni.

اسم الكتاب: مختصر كتاب الأصول الثلاثة


تأليف: صالح بن فوزان الفوزان


الناشر: المكتب التعاوني للدعوة وتوعية الجاليات بالربوة


نبذة مختصرة: كتاب مترجم إلى اللغة السواحيلية، عبارة عن مختصر لكتاب مختصر كتاب الأصول الثلاثة، لفضيلة الشيخ الإمام صالح بن فوزان الفوزان - حفظه الله -، يبين فيه أهمية العلم والأمور الأربعة التي يجب على كل مسلم معرفتها.


Masomo katika umuhimu wa Tawheed.
Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah

< Swahili >

kiswahili

        
Mtunzi:
Imamu Sheikh Saleh bin Fauzan Al-Fawzan.



Mfasiri:
 Yasini Twaha Hassani.
Abubakari Shabani Rukonkwa.


 
Kimerejewa na:
Yunus Kanuni Ngenda
 
 

الدروس في أهمية التوحيد
مختصر كتاب الأصول الثلاثة.
السواحلية

المؤلف:
فضيلة الشيخ:  فضيلة  الشيخ  الإمام صالح بن فوزان الفوزان.

المترجم:
ياسين طه حسن
أبوبكر شعبان ركونكوا.

المراجع:
يونس كنون نغندا

 

 

 

 


YALIOMO:

1.Elimu.
2.Mambo manne ambayo nilazima kwa muislam kujifunza.
3.Maana ya subra na vigawanyi vyake.

 

 

 

 

 

 

MASOMO KATIKA UMUHIMU WA TAWHIID
Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah


Utangulizi:
   Kaanza kwa kusema Bismi llahi Rrahmani Rrahim; Kwajina la Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma mwenye kurehemu.
Ameanza Mwenyezi Mungu Amrehemu risala hii kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma mwenye kurehemu, kwa kufuata kitabu cha Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu, kwa sababu macho yako yakiangalia ndani ya msahafu na kabla ya kila sura kuna (Bismi llahi Rrahmani Rrahim).
Kuanzia neno hili katika risala na katika vitabu nikufuata kitabu cha Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu, vilevile nabii Muhammad (s.a.w) Alikua -ana mwambia muandishi- a'ndike mwanzo wa kila barua wakati anapo watumia viongozi na maraisi na waliyoko mbali ana walingania katika Uislamu, anaanza kuandika:
   Kwajina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma mwenye kurehemu.
Na alikua Mtume (s.a.w) anaanza mazungumzo yake na maneno yake kwa: Bismi llahi Rrahmani Rrahim, yaonyesha kuanza kwa Bismi llahi Rrahmani Rrahim ni sunna ya Mtume (s.a.w), vilevile Nabii Sulaiman (s.a.w) alipo muandikia Malkia -Mfalme wa saba' Yemen- ameanza kuandika kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma mwenye kuruhemu: (Malkia akasema: Enyi wahishimiwa! Hakika nimeletewa barua tukufu* Imetoka kwa Sulaiman nayo ni:
Kwajina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye kurehemu* Msinifanyie jeuri, na fikeni kwangu nanyi mmekwisha kuwa wenye kusalimu amri).
 (An-Naml: 29-31).
Inatakiwakuanza na jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye kurehemu, katika kila jambo lenye umuhimu, na katika kila kitabu chenye umuhimu na thamani, na katika kila risala.
Kwa sababu hii wale ambao hawaanzi kwenye vitabu vyao na risala zao kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye kurehemu, hao wameacha sunna ya Mtume na kuto kufuata kitabu cha Mwenyezi Mungu Mshindi na mtukufu, huenda kwa sababu hiyo vitabu vyao na risala zao hazina baraka na ndani yake hakuna faida; kwa sababu ikiwa hakuna jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye kurehemu huondolewa faida.

Risala ya kwanza    Maswala manne ambayo yameambatana na Surati Al-Asr,

ILIMU
Tambua Mwenyezi Mungu akurehemu.
Hili ni neno linalo ashiria umuhimu wa mada, anapo sema: Tambua: lina maana ya kwamba atakacho kwambia nimuhimu sana.

MWENYEZI MUNGU AKUREHEMU:
Hii ni dua kwa mtafutaji wa Ilimu, anawaombea watafutaji wa elimu Mwenyezi Mungu awarehemu, na awape rehma zake, maneno haya ndani yake kuna upole kutoka kwa mwalimu kwenda kwa mwanafunzi, na kwamba yeye anaanza kwa maneno mazuri na dua njema, mpaka awaathiri kwa maneno hayo na wamuelekee mwalimu wao.

  Lakini mwalimu akianza maneno kwa ukali na maneno yasio faa jambo hili lina wakimbiza -wanafunzi-, wajibu wa mwalimu na wale wanao lingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, na nijuu ya yule anae amrisha mema na kukataza mabaya kuwa mpole kwa yule anae ongea nae, kwa kumuombea dua na kumsifu kwa maneno laini, kwani hili lapelekea kukubali.
Lakini mtu mwenye kiburi mjeuri, yeye ana maneno maalumu, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
 (Wala msijadiliane na watu wa kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake).
(Al-Ankabut: 46).

Wake walio dhulumu nafsi zao miongoni mwa walio pewa kitabu, wakafanya ujeuri na kiburi, hao hawalinganiwi kwa upole, wao hulinganiwa kwa ukali. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
(Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na wakazanie. Na makaazi yao ni Jahannamu, na huo ndio mwisho mbaya).
 (At-Tawba: 73).

Wanaafiki hawajadiliwi kwa silaha, lakini hujadiliwa kwa hoja na maneno makali, nakuwatahadharisha watu wasiwe karibu nao, na Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na uwaambie maneno ya kuathiri na kuingia katika nafsi zao).
(An-Nisaa: 63).

 

 Hao wana maneno yao maalumu; kwa sababu wao ni wapingaji wenye viburi, wala
hawataki haki bali wanataka kuwapoteza watu, hao huambiwa kwa wanayo stahiki.

NILAZIMA JUU YETU KUJIFUNDISHA MAMBO MANNE.

     Jambo hili sio hiyari, wala sio lenye kupendeza -ukitaka unafanya hukutaka unaacha- isipo kua ni lazima hasa.
Tutapo acha kujifundisha mambo haya kwa hakika tuna pata madhambi, kwa sababu jambo hili ni lazima, hakusema: ni hiyari kwetu au yapendeza kwetu, lakini kasema: ni lazima kwetu, na jambo lazima maana yake: mwenye kuliacha hupata dhambi, na kwa sababu elimu haipatikani isipo kuwa kwa kujifundisha, na kujifundisha kuna hitaji umuhimu na juhudi na muda, na kuna hitaji ufahamu na kuhudhurisha moyo, huku ndiko kujifundisha.

Mwenyezi Mungu Anasema katika Suratul Asr: kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma mwenye kurehemu (Naapa kwa Zama!* Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara* Isipokuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri).
(Al-Asr: 1-3).

MAS'ALA MANNE:
yaani upekuzi, yameitwa mas'ala; kwa kuwa mambo hayo nilazima kuulizwa na kutiliwa umuhimu.

JAMBO LA KWANZA: ILIMU.
    Ilimu: makusudio ya ilimu hapa ni elimu ya kisheria; kwa sababu ndio ambayo ni lazima kujifundisha, na mas'ala haya ni lazima kujifundisha kwa kila Muislam, mwanamume au mwanamke, alie huru au mtumwa, tajiri au maskini, mfalme au raiya. Kila Muislam ni lazima kwake kujifundisha mas'ala haya manne.
      Na hili ndio linaloitwa na wanachuoni Ulazima waki pekee, ndio ambao ni lazima kwa kila mmoja katika Waislam, swala tano kwa wanamume na wanawake, na swala ya jamaa misikitini kwa wanamume. Jambo hili ni lazima kwa kila Muislam kujifundisha, kwa sababu hiyo alisema: ni lazima juu yetu, na hakusema: ni lazima kwa baadhi yetu, ila kasema: ni lazima juu yetu, yaani sisi Waislam, hii nikatika elimu ambayo ni lazima kwa kila mtu; kwa sababu elimu zipo namna mbili: Jambo la kwanza ambayo ni lazima kwa kila mtu kujifundisha, hakuna udhuru kwa asiye jifundisha, nayo niile ambayo haisimami dini bila yenyewe, mfano nguzo za Uislamtano  ambazo ni:
A.Shahada mbili,
B.kusimamisha Swala,
C.kutoa Zaka,
D.kufunga Mwezi mtukufu wa Ramadhani,
E. Kuhiji nyumba ya Mwenyezi Mungu,
 
Haifai kwa Muislam kuto jua mambo haya ni lazima kujifundisha.
Kwa sababu kujifundisha maana ya Shahada mbili ndiko kujifundisha Tauhidi, anajifundisha Muislam tauhidi ili aifanyie kazi, na ajifundishe yanayo kwenda kinyume na tauhidi ili ajiepushe nayo, haya ndio mafungamano ya Shahada mbili, vilevile ajifundishe nguzo za swala na sharti zake, na yalio yalazima ndani ya swala, na sunna za swala.

Vilevile ajifundishe hukumu za zaka, na ajifundishe hukumu za funga, na ajifundishe hukumu za hija, anapotaka kuhiji ni lazima ajifundishe hukumu za hija na hukumu za umra, ili atekeleze ibada hizi katika njia ilio amrishwa.
Na kipengele hiki hakuna udhuru kwa yeyote kuto kijua, nacho kinaitwa ulazima wa kila Muislam.

Sehemu ya pili katika vigawanyo vya elimu: nayo ni tofauti na elimu ya kisheria ambayo umma unaihitaji kwa ujumla wake, nasio kila mtu huihitaji, mfano hukumu za kuuza na kununua na hukumu za muamala, na hukumu za kutoa wakfu,na mirathi na usia, na hukumu za kuoa, na hukumu za makosa ya jinai, mambo haya nilazima kwa umma; lakini sio lazima kwa kila mtu kujifundisha, isipokuwa watapo jifundisha wenye kutosheleza na malengo yakatimia miongoni mwa wanachuoni yatosha; jambo hili linaitwa: faradhi kifaya, wakifanya baadhi ya watu madhambi huondoka kwa wengine, na watapo liacha wote basi hupata dhambi wote.

Ilimu ya lazima ndio ambayo ataulizwa mja siku ya kiyama, kwa nini hukujifundisha? Kwa nini hukuuliza? Ilimu ambayo ataisema pindi atapo wekwa ndani ya kaburi: Mola wangu ni Mwenyezi Mungu, na Uislam ndio dini yangu, na nabii wangu ni Muhammad (s.a.w) jambo hili laokoa, ataambiwa: umejifundisha wapi? Atasema: nimesoma kitabu cha Mwenyezi Mungu na nikajifundisha.

Ama Yule alie jitenga mbali na elimu hiyo kwa hakika atapo ulizwa katika kaburi lake atasema: hahahaha sijuwi niliwasikia watu wakisema jambo Fulani nami nikalisema.
Mtu kama huyu atawashiwa moto ndani ya kaburi lake -Allah atunusuru- na kaburi litambana hadi mbavu zake hupishana, na kaburi lake huwa ni shimo miongoni mwa mashimo ya moto wa Jahannam; kwa sababu yeye hakutaka kujifundisha wala kusoma, ataambiwa:
(Hukutaka kujifundisha wala kusoma).

Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kwa ufupi kwa hadithi ya Anas (1338) na kaipokea pia Imam Muslim kwa ufupi hadithi ya Anas (r.a) (2870).
Na kaipokea Abuudaud kwa hadithi ya Bara' bin A'zib (r.a) kwa urefu (4752).
Yeye hakujifundisha, wala hakuwafuata wanachuoni, bali yeye kapoteza uhai wake, huyu ndio ambae atakua sehemu mbaya -Allah atunusuru.

ILIMU: Hii ndio ilimu ya kisheria, kinacho takiwa kwa ujumla wetu na mmoja mmoja nako nikumjua Mwenyezi Mungu kwa Majina yake na Sifa zake, na kujua haki zake juu yetu, nayo ni Kumuabudu yeye peke yake hana mshirika katika u'ngu wake, jambo la kwanza kulitambua mwanadamu ni kumjua Mola wake Mtukufu, na namna ya kumuabudu.

NA KUMJUA MWENYEZI MUNGU, NA KUMJUA MTUME WAKE.

KUMJUA MWENYEZI MUNGU:
  Vipi mja atamjua Mola wake? Atamjua kwa alama zake na viumbe wake, miongoni mwa alama za kumjua kwake: usiku na mchana, na katika viumbe vyake: jua na mwezi, kama tunavyo bainisha hapa kwa matakwa ya Allah.
Hujulikana Mwenyezi Mungu kwa alama zake za kidunia na Aya zake za qur-ani. Anapo soma qur-ani, humtambua Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba yeye ndio ambae kaumba mbingu na ardhi, naye Mwenyezi Mungu ndie ambae kavifanya kuwa vyepesi vilivyoko mbinguni na ardhini, naye Mwenyezi Mungu ndie ambae Ana huisha na kufisha, naye nimuweza juu ya kila kitu, naye ni Mwingi wa rehma mwenye kurehemu, Qur-ani ina mtambulisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, naye Mwenyezi Mungu ndie ambae Ametune'mesha ne'ma zote, naye Mwenyezi Mungu ndie Alie tuumba na kuturuzuku, utapo soma qur-ani utamjua Mola wako Mshindi na Mtukufu kwa Majina yake na Sifa zake na vitendo vyake.

Na utakapo angalia katika hii dunia utamtambua Mola wako Mtukufu kama yeye ndie alie umba, na akafanya  wepesi katika huu ulimwengu na akaupitisha kwa hikma yake na kwa Ujuzi wake, Hii ndio Elimu ya kumjua Mwenyezi Mungu Mtukufu.

NA KUMJUA MTUME WAKE:
Yeye ni Muhammad (s.a.w) kwa sababu yeye ni Mwenye kufikisha niaba ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yeye niwakati baina yetu na Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kufikisha ujumbe, hapana budi kumjua, unafahamu yeye ni nani? Unafahamu ukoo wake?
na ujuwe mji wake, na ujuwe aliyo kuja nayo (s.a.w) unafahamu namana Wahyi ulivyo anza kushuka? Na namna alivyo simama katika kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu katika mji wa Makkah na Madina, unajua hestoria ya mjumbe wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) japo kwa ufupi?.
Mtume (s.a.w) yeye ni Muhammad bin Abdullah bin Abdul muttwalib bin Hashim bin Abdi manafi mpaka mwisha wa nasabu ya mtume mtukufu ambayo inaishia kwa NaBii Ibrahim (s.a.w), na unajua namna alivyo ishi kabla ya utume, na namna alivyo jiwa na wah'yi kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na nini alicho fanya (s.a.w) baada ya kupewa utume, utayajua yote hayo kwa kusoma hestoria yake (s.a.w). na haifai kwa Muislam kutomjua mtume (s.a.w) vipi unamfuata mtu hali yakua humjuwi?! Haiingii akilini.

NA KUIJUA DINI YA KIISLAM.
Kuijua dini ya kiislam: ambayo ndio dini ya huyu Mtume (s.a.w) bali ndio dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ambae kawaamrisha kwa dini hiyo waja wake, naye ndio ambae amekuamrisha kuifuata, na wewe watakiwa kuifuata, hapana budi kuijua hii dini, na Uislam ndio dini ya Mitume wete. Mitume wete dini yao Uislam kwa maana ya ujumla, yeyote alie mfuta Mtume miongoni mwa Mitume huyo ni Muislam mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu mwenye kumfuata yeye, mwenye kumpwekesha yeye.

 Huu ndio Uislam kwa maana ya ujumla, hakika ni dini ya Mitume wote, Uislam nao ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa tauhidi, na kumfuata yeye kwa kutii, na kujiepusha na ushirikina na watu wake.
Ama Uislam kwa maana yake halisi niule ambao amemtuma nao Mwenyezi Mungu Mtume wake Muhammad (s.a.w) kwa sababu baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) hakuna dini isipokuwa dini yake (s.a.w), na Uislam umehusishwa katika kumfuata yeye (s.a.w) haiwezekani Yahudi akasema: Mimi ni Muislam, au Naswara aseme: Mimi Muislam baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) haliyakua hamfuati, Uislam baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) ni kumfuata, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni.
)Al-Imran: 31).

Huu ndio Uislam kwa maana ya ujumla na kwa maana yake halisi.

KWA DALILI.
Kwa dalili: sio kwa kuiga lakini kwa dalili katika Qur-ani na Sunna, hii ndio elimu.
Amesema Ibnul-QaYyim katika kitabu chake Al-kafiyatu shafiya:                                                                                   Ilimu kasema Mwenyezi Mungu kasema Mtume wake kasema Swahaba hao ndiyo wajuzi Siyo elimu inayo sababisha tofauti za kijinga kati ya Mtume na maoni ya Fulani, hii ndio elimu.
Elimu ni ile elimu ya kitabu(Quraan) na sunna, na kuhusu maneno ya wanachuoni yenyewe husherehesha na kuweka wazi zaidi maneno ya Mwenyezi Mungu na maneno ya Mtume wake (s.a.w)
Na kwa hakika ndani ya maneno hayo au baadhi yake huwa kuna makosa.

KUIFANYIA KAZI ELIMU

JAMBO LA PILI: KUIFANYIA KAZI.
      Kuifanyia kazi, maana yake: kwa elimu kwa sababu mwanadamu anafundisha na ana jifundisha hapana budi kuifanyia kazi elimu yake, elimu bila matendo itakua ni hatari kwa mwenye nayo, haiwi elimu yenye manufaa ila kwa matendo, ama Yule alie jifundisha na hakuifanyia kazi elimu yake huyo kakasirikiwa; kwa sababu yeye kaijuwa haki na akaiacha kwa elimu.
Mtunzi  anasema: (Na Mwanachuoni hakuifanyia kazi elimu yake Ataadhibiwa kabla ya wenye kuabudia Masanamu).

Na jambo hili limetajwa kwenye hadithi tukufu: (Mtu wa mwanzo kuingizwa katika moto siku ya kiyama, Mwanachuoni ambae hakuifanyia kazi elimu yake(.
Kapokea hadithi hii Imam Tirmidhi (2382).
nayo ni hadithi ndefu ndani yake: (Hao wenye sifa tatu ndio wa mwanzo kabisa kuingizwa katika moto siku ya kiyama), hadithi ya Abaa huraira (r.a).
Elimu imeambatanishwa na vitendo, na vitendo ndio matunda ya elimu, elimu bila vitendo ni kama mtu bila matunda, hauna faida ndani yake, na elimu imeletwa ili ifanyiwe kazi.

Kama yalivyo matendo yasio kua na elimu inakua ni msiba na upotevu kwa mtendaji.
Ikiwa mwanadamu anafanya matendo bila elimu kwa hakika matendo yake yana kuwa ni msiba na tabu kwa mtendaji, Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w):
(Yeyote atakae fanya Amali hakuna Amri yetu yatakuwa ni yenye kurejeshwa).

Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kabla ya hadithi (7350), na Muslim (18/1718), hadithi ya Bibi Aisha (r.a), na kapokea Bukhari (2697) na Muslim (17/1718) kutoka kwa Bibi Aisha (r.a) Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w): (Yeyote atakae zua katika dini yetu hii jambo lisilo kuwemo atarejeshewa).
Na kwa sababu hii tuna soma katika suratul Fatiha katika kila raka: (Tuongoze njia iliyo nyooka* Njia ya wale ambao uliyo waneemesha, siyo ya wale waliyo kasirikiwa na wala waliyo potea).
 (Al-Fatiha: 6-7).

Akataja Mwenyezi Mungu wale ambao wanafanya bila elimu walio potea, na wale ambao wanafahamu na hawayafanyii kazi wamekasirikiwa, tuzindukane na jambo hili kwa sababu ni muhimu sana.

KULINGANIA KATIKA ILIMU.
JAMBO LA TATU: KUILINGANIA KWAKE.
Kuilingania katika njia ya Mwenyezi Mungu: maana yake: haitoshi kujifundisha mwanadamu na akafanya pekeyake, wala asilinganii katika njia ya Mwenyezi Mungu Mshindi na Mtukufu, hapana budi awalinganie wengine, ili ainufaishe nafsi yake na nafsi za wengine, na kwa sababu elimu hii ni amana, sio milki yako ukawa unailimbikiza tu na una wanyima watu, na watu wana shida nayo, ilio wajibu kwako kufikisha na kubainisha na kuwalingania watu katika kheri, hapana budi kuifikisha na kuibainisha kwa watu.                                               Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na pindi Mwenyezi Mungu alipo funga ahadi na walio pewa Kitabu kuwa: Lazima mtawabainishia watu, wala hamtokificha). (Al-'Imran: 187). Ahadi hii kaichukua Mwenyezi Mungu kwa Wanachuoni wawabainishie watu yale walio fundishwa na Mwenyezi Mungu ili waeneze kheri, na wawatowe watu katika gize kuwaweka katika nuru, Hii ndio kazi ya Mitume (s.a.w) na wafuasi wao, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Sema: Hii ndiyo njia yangu ninalingania kwa Mwenyezi Mungu kwa ilimu mimi na wanao nifuata.

Na ametakasika Mwenyezi Mungu! Wala mimi si katika washirikina). (Yusuf: 108).

Hii ndiyo njia ya Mtume (s.a.w) na nhia ya wafuasi wake, ilimu na matendo na kulingania kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, yeyote asie lingania haliyakuwa anao uwezo wa kulingania na ilimu anayo akaificha, kwa hakika atafungwa kamba za moto mdomoni mwake siku ya kiyama kama ilivyo katika hadithi. Kaipokea Abuu daudi (3658), na Tirmidhi (2649), na Ibnu Maja (261) na (266) hadithi ya Abaa huraira (r.a) Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w): (Yeyote atakae ulizwa katika mambo ya ilimu akaficha, atafungwa kamba na Mwenyezi Mungu za moto mdomoni mwake siku ya kiyama). Na Ibnu Maja (265) kwa hadithi ya Abii Saidi l-khudri (r.a) Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w): (Yeyote atakae ficha Elimu katiaka Elimu anazo wanufaisha Mwenyezi Mungu watu, mambo ya dini, Allah atamfunga siku ya kiyama kamba za moto mdomoni mwake).

KUFANYA SUBRA JUU YA MAUDHI YANAYO PATIKANA NDANI YAKE.

JAMBO LA NNE:
KUFANYA SUBRA JUU YA MAUDHI YANAYO PATIKANA NDANI YAKE.
Subra juu ya maudhi yanayo patikana ndani yake:
kama inavyo julikana yeyote ane walingalia watu aka waamrisha mema na aka kataza mabaya, kwa hakika atafikwa na maudhi kwa watu waovu; kwa sababu watu wengu hawapendi kheri, bali hupenda matamaniyo na haramu na matakwa ya nafsi yaliyo mabaya, anapokuja mwenye kuwalingania kwa Mwenyezi Mungu, na kukemea matamanio yao, hapana budi.

 

Miongoni mwao kufanya vibaya ima kwa maneno au kauli,     
Ni lazima juu ya mwenye kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu na kutaka radhi za Mwenyezi Mungu asubiri maudhi, na aendelee katika kulingania, na kiigizo chake ni Mitume (s.a.w) na mbora wao na wa mwisho wao Muhammad (s.a.w).

Yamemfika mangapi kutoka kwa watu? Na maudhi mangapia kayapata kwa maneno na vitendo? Walisema: mchawi, muongo, wakasema: mwandawazimu. Wakasema dhidi yake maneno ambayo ameyataja Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani ya   Qur-ani, wakamfanyia maudhi, kapigwa mawe mpaka miguu yake ikatoa damu (s.a.w) wakati alipo walingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, kawekewa utumbo wa ngamia juu ya mgongo wake akiwa ana sujudu mbele ya Alkaaba, kaahidiwa kuuliwa katishwa, katika vita vya Uhudi ali dhuriwa yeye na maswahaba zake (s.a.w),
kavunjwa memo yake manne ya mbele, kapasuliwa kichwani mwake (s.a.w) kasukumwa ndani ya shimo, haliyakuwa ni nabii wa Mwenyezi Mungu, madhara yote haya kayapata katika kulingania kwaajili ya Mwenyezi Mungu, lakini yeye kasubiri kavumilia haliyakua ndio mbora wa viumbe wote (s.a.w), hapana budi kwa Yule anae fanya kazi ya kulingania kufikwa na maudhi kiasi cha imani yake na dawa wake; pamoja na yote hayo yatakiwa asubiri, akiwa yupo katika haki, asubiri avumilie, yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu na maudhi yanayo mfika yatakuwa katika mizani yake mema mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Mambo haya ma nne nilazima tujifundishe kwa urefu,
Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Naapa kwa Zama!).
(Al-Asr1).
 Ameapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa zama na wakati nao ni kiumbe, na Mwenyezi Mungu Mtukufu anaapa kwa anacho kitaka miongoni mwa viumbe, na kiumbe haapi isipokuwa kwa jina la Mwenyezi Mungu, Na Mwenyezi Mungu haapi isipokuwa kwa kitu chenye umuhimu, na ndani yake kuna alama miongoni mwa alama zake, Utakasifu niwake na ametukuka, ndani ya zama kuna mazingatio na umuhimu, na kwa sababu hiyo Ameapa Mwenyezi Mungu kwa muda wa Laasiri, na kwa usiku unapo funika na akaapa kwa mchana. Ama kiumbe haifai kuapa isipokua kwa jina la Mwenyezi Mungu, na haifai kwetu kuapa kwa asie kua Mwenyezi Mungu, Amesema Mtume (s.a.w): (Yeyote atakae apa kwa asiye kua Mwenyezi Mungu kwa hakika amekufuru au ameshirikisha). Kapokea hadithi hii Imam Abuu daudi (3251), na Tirmidhi (1535) kwa hadithi ya Ibni Omar (r.a).
Na Akasema: (Yeyote anae taka kuapa Aape kwa jina la Mwenyezi Mungu au akae kimya).
Kapokea hadithi hii Imam Bukhari (6108), na Muslim (1646) kwa hadithi ya Ibni Omar (r.a).

NI LIPI JIBU LA KIAPO?
    Ni kauli yake: (Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika hasara).
(Al-Asr: 2).
Mwanaadamu Binaadamu woote hakuvuliwa hata mmoja siyo wafalme wala maraisi, wala matajiri, wala
Mafakiri, wala walio huru, wala watumwa, wala wanamume wala wanawake, kila binaadamu yupo katika Hasara, maana yake: katika hasara na maangamio ikiwa wataupoteza huu muda ulio wa thamani, wakautumia katika kumuasi Mwenyezi Mungu, na katika yanayo wadhuru.
Wanaadamu weete wamo ndani ya hasara na maangamio isipokuwa atakae sifika na sifa nne nazo: Ilimu, na Matendo, na kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, na kufanya subra juu ya maudhi.
Yeyote atakae sifika na sifa hizi nne ameokoka katika hii hasara. Wala haiwezekani kumuamini Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa Ilimu, Ambayo ndio kumjuwa Mwenyezi Mungu.
(Na wakatenda mema). (Al-Asr: 3).
Maana yake: wamefanya matendo yalio mazuri katika mambo ya lazima na yasio yalazima, wakatumia muda wao kwa matendo mema
kwa yale yanayo wanufaisha katika dini yao na dunia yao.
   Hata matendo ya kidunia ndani yake kuna ujira ikiwa utakusudia katika hayo matendo kuwa ni sababu ya kufanya twaa, itakuwaje matendo kwaajili ya akhera, lamsingi jitahidi usipoteze muda utumie katika mambo yanayo kunufaisha na yanayo kufiidisha.
)Na wakausiana kwa haki). (Al-Asr: 3).
Wameamrisha mema, na Wamekataza mabaya, na Wakalingania katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na Wakafundisha Ilimu yenye manufaa, na Wakazagaza Ilimu na kheri kwa watu.
Wakawa walinganiaji katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
)Na wakausiana kusubiri). (Al-Asr: 3).
Walifanya subra kwa yale walio yapata,
Na Subra katiak lugha ya kiarabu: kuziwia, lakini makusudio hapa: kuiziwia nafsi katika kumcha Mwenyezi Mungu.
Nazo zipo aina tatu:
1. Kufanya subra katika kumtii Mwenyezi Mungu.
2.Kufanya subra kwa yale aliyo kataza Mwenyezi Mungu.
3.Kufanya subra juu ya makadara ya Mwenyezi Mungu.

1.Subra katika kumtii Mwenyezi Mungu, kwa sababu nafsi inapenda uvivu na inapenda raha, hapana budi kuizoweza binaadam nafsi juu ya kutii na kusali na kufunga na kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu japokuwa mambo haya nafsi haiyapendi, anaiziwiya katika utiifi wa Mwenyezi Mungu.

2.Kufanya subra kwa yale aliyo kataza Mwenyezi Mungu.   
Nafsi inataka mambo ya haramu, na mambo ya matamanio, inaelekea huko na kuvutiwa sana, hapana budi aifunge na kuiziweya katika mambo ya haramu, jambo hili lahitaji subra, na siyo jambo rahisi kuizuiya nafsi katika mambo ya matamanio ya haramu, ambae hana subra kwa hakika nafsi yake itamshinda na itamvuta kwenye haramu.

3.Kufanya subra juu ya makadara ya Mwenyezi Mungu yenye kuu miza.
Matatizo yanayo mpata mwanaadamu kwa kufiliwa na mtu wake wa karibu, au kupoteza mali, au maradhi yanayo mpata mwanaadamu, hapana budi afanye subra juu ya hukumu na makadara ya Mwenyezi Mungu, asikate tamaa wala kuchukia, bali auziwiye ulimi na kuto omboleza na kutokata tamaa, na aiziwiye nafsi kutokata tamaa, na aziwiye viungo na kuto jipiga makofi na kuchana nguo kwa hasira, Hii ndiyo subira wakati wa matatizo.

Kuhusu maasi asifanyi subra juu yake bali atubiye kwa Mwenyezi Mungu na ayakimbiye; lakini wakati wa mitihani ambayo hukuingia ndani yake, bali nikutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amekukadiria juu yako na kukupa mtihani au adhabu kwako kutokana na madhambi uliyo yafanya, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
(Na misiba inayo kupateni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi). (Ash-Shura: 30).
Utapofika msiba kwa Muislam katika nafsi yake au mali zake au watoto zake au ndugu wa karibu au yeyote kati ya ndugu zake Waislam ni juu lako kufanya subra na kutegemea malipo kwa Mwenyezi Mungu.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
(Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea *  Hao juu yao zitakuwa Baraka zitokazo kwa Mola wao Mlezi na rehema. Nao ndio wenye kuongoka).
 (Al-Baqara: 156-157).

Hii ndio subra, na mfano wake kufanya subra juu ya maudhi unayo yapata katika kulingania neno la Mwenyezi Mungu Mtukufu hayo nikatika matatizo, nilazima ufanye subra kwa hayo unayo yapata katika njia ya kheri, Nawala usiachi kufanya kheri; kwa sababu baadhi ya watu wanataka kufanya kheri lakini akikutana na jambo linalo chukiza anasema: sio lazima juu yangu kuiweka nafsi yangu kwenye mambo kama haya, kisha anaacha kufundisha ikiwa ni mwalimu, anaacha kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, anaacha kuongea ikiwa ni khatwibu wa muskiti, anaacha kusalisha muskitini, anaacha kuamrisha mema na kukataza mabaya,  Huyu hakusubiri kwa aliyo yapata miongoni mwa maudhi.
Amesema Imam Shaafy (r.a):
"Laiti Mwenyezi Mungu asinge teremsha dalili kwa waja wake ila surahii  ingeliwatosha".

Kwa hakika kanukuu Imam Shafy: yeye ni Muhammad ibni Idrisa Ashaafy nasabu kwa babu yake wa nne jinalake shafy, nae ni mkuraishi, katika familia ya mutw-labi, kafariki mwaka (204) h.j.r. naye ni mmoja kati ya Maimamu wa nne, na akasema maneno haya kwa sababu Mwenyezi Mungu kabainisha kwanye sura hii sababu za kupotea na sababu za kuongoka
.
Kuhusu sababu za kuongoka: Asifike mwanaadamu na hizi sifa nne: Ilimu, na Matendo, na Kulingania, nakufanya subra juu ya maudhi yanayo tokea katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ikasimama hoja kutoka mwa Mwenyezi Mungu juu ya waja wake kwa sura hii, Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ana waambia: Hakika mimi Allah nime kubainishieni sababu za kuokoka katika sura hii fupi sana.
Na Qur-ani yate pamoja na Sunna vime fafanuwa zaidi mambo haya ma nne, lakini sura hii imebainisha sababu za kuongoka kwa ujumla, ikasimama hoja kwa viumbe, na zikabaki dalili ndani ya qur-ani na sunna ziki fafanuwa zaidi na kuweka wazi mambo haya ma nne, na wala sio makusudio ya Imam Shafy kwamba sura hii yawatosha watu, kama asingeliteremsha Mwenyezi Mungu sura tofauti na hii, lakini hoja imesimama juu yao; kwa sababu Mwenyezi Mungu kisha bainisha ndani yake sababu za kuokoka na sababu za uongofu, asitokei yeyote siku ya kiyama akasema:
Mimi sijuwi sababu za uongofu wala sijuwi sababu za kupotea naye akisoma sura hii fupi sana.

NA AKASEMA IMAMU BUKHARI (r.a): MLANGO UNAO ELEZEA ILIMU KABLA YA KAULI NA MATENDO.
Na dalili: (Basi jua ya kwamba hakuna Mungu anayefaa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa dhambi zako na za Waumini wanaume na Waumini wanawake). (Muhammad: 19).
Akaanza Ilimu kabla ya kauli na matendo.
Bukhari: yeye ni Muhammad bin Ismail bin Imrahim   Al-Bukhary, kanasibishwa na Bukhara mji uliyoko Mashariki, ni Imam wa Hadithi bingwa wa kuhifadhi (r.a), mtunzi wa (Swahihi) kitabu ambacho kina usahihi baada ya kitabu cha Mwenyezi Mungu.

Ilimu kabla ya kauli na matendo; kwa sababu matendo hayanufaishi isipokuwa yakijengewa juu ya ilimu, lakini matendo yaliyo jengeka juu kutenda.
Na dalili: kuhusu kichwa cha habari kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Basi jua ya kwamba hakuna Mungu anayefaa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa dhambi zako). (Muhammad: 19).

Hakika kaanza na Ilimu, Na kauli ya ujinga kwa hakika hayamnufaishi mwenye nayo bali ni hasara kwake na upotovu juu yake siku ya kiyama, hapana budi atangulize kujifundisha kabla ya yake Tukufu: (Na omba maghufira) hii ndio Amali, Akaanza Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Elimu kabla ya amali; kwa sababu matendo yakiwa niya kijinga hakika hayamnufaishi mwenye nayo, Aanze mwanaadamu na Elimu kwanza kisha afanye yale aliyo jifundisha, huu ndio msingi wa dini ya uislam.

 


Utangulizi:
Kila sifa kamilifu niza Mwenyezi Mungu muumba wa vitu vyote sala na amani ziwe juu ya kipenzi cha Allah mtume wetu Muhammad (s.a.w) ambae ametuwa akiwa nirehma kwa walimwengu wote akiwa nimwenye kubashiri pepo na kukhpfisha moto, na ziwe juu ya maswahaba zake wote waongofu na wote watakao fuata muongozo wake mpaka siku ya qiyama.

Kitabu hiki ni muendelezo wa sehemu ya kwanza ya kitabu kilicho tangulia tukiwa tunaendelea kunufaika na maneno alio andika imamu Imamu Sheikh Saleh bin Fauzan Al-Fawzan. Mwenyezi Mungu amhifadhi.

RISALA YA TATU MAMBO MATATU NI LAZIMA MUISLAM AJIFUNDISHE NA AYAFANYIE KAZI.   
  Tambua Mwenyezi Mungu akurehemu ya kwamba nilazima juu ya kila Muislam wa Kiume na Wakike kujifundisha mambo haya matatu na kuyafanyia kazi.
TAMBUA: ni neno ambalo huletwa kwaajili ya umuhimu wa kinacho elezwa baadae, na maana yake: jifundishe na ufahamu na uwe na yakini.


MWENYEZI MUNGU AKUREHEMU: Hii ni dua kwako ya rehma, na hili pia limekwisha tangulia kwamba mwalimu yatakiwa awe mpole kwa mwanafunzi, na amuombee dua na kumuhimiza, kwa sababu haya nikatika njia bora za kufundisha, na wala haifai kwake kumkabili kwa ukali na uzito na chuki, kwa sababu haya nanapelekea achulie Elimu, pia yaonyesha nasaha ya mwanachuoni, na kwamba yeye anachotaka ni nasaha na kuelekeza na usawa.
NI LAZIMA: Yaonyesha kwamba jambo hili siyo hiyari, anaetaka anafanya na asietaka anaacha, bali ulazima hapa ni katika namna ya mkazo kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na siyo ulazima kutoka kwa mwanachuoni, bali ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa yale aliyo yateremsha katika Kitabu na Sunna, katika kuwalazimisha waja kwa mambo haya.

NI LAZIMA JUU YA KILA MUISLAM WAKIUME NA WAKIKE,
    Maana yake: ni lazima juu yakila mwanamume na mwanamke miongoni mwa Waislam sawasawa wakiwa huru au watumwa au wanaume au wanawake, kwa sababu mwanamke hushirikiana na mwanaume kwenye mambo ya lazima mengi sana, isipokuwa yale yanayo wahusu wanaume pekeyao kwa dalili inayo wahusu wao tu, mfano: ulazima wa swala za jamaa misikitini, swala za ijumaa, na mfano wa kuzuru makaburi mambo haya ni haswa kwa wanaume, na mfano wa kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, sababu jambo hili ni maalumu kwa wanaume.

MAMBO MATATU:  
Kujifundisha maana yake hapa: kupata elimu kutoka kwa wanachuoni na kuhifadhi na kufahamu na kudiriki mambo sawasawa, hii ndiyo elimu, nawala siyo makusudio kujisomea tu ovyo au kutwalii tu.
Na haifai kujifundisha kwenye vitabu kama hali ya zama tulizo nazo, kwa sababu kujifundisha kwa kutumia vitabu ni hatari sana, hupatikana madhara makubwa,  na kufundishana -kwanjia hiyo ya vitabu- kuna dhuru zaidi kuliko mjinga; kwa sababu mjinga anatambuwa kama yeye ni mjinga na husimama kwenye kiwango chake, lakini mwenye kujifundisha hujiona ya kwamba ni mjuzi, ana halalisha aliyo ya haramisha Mwenyezi Mungu, na ana haramisha aliyo ya halalisha Mwenyezi Mungu, na anaongea na husema juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu, ni mambo hatari sana.
Elimu haichukuliwi kutoka kwenye vitabu moja kwa moja, isipokuwa vitabu ni nyenzo tu, lakini uhakika wa elimu huchukuliwa kutoka kwa wanachuoni ambao wapo katika njia ya wema walio tangulia vizazi kwa vizazi, na vitabu ni nyenzo za kutafutia elimu.

 

 


KUAMINI YA KWAMBA:
A.MWENYEZI MUNGU AMETUUMBA.
B. ANATURUZUKU.
C. HAKUTUACHA BURE.                                                                                          
Mwenyezi Mungu ametuumba na kuturuzuku na hajatuacha bure.
1:kwamba Mwenyezi Mungu ametuumba, maana yake: Ametuweka baada ya kuto kuwepo, sisi kabla yakutuumba hatukuwa chochote, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika ulimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinachoweza kutajwa). (Al-Insaan: 1).
Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Akasema: Ndio hivyo hivyo amesema Mola wako: Haya ni rahisi kwangu. Na hakika Mimi nilikwisha kukuumba wewe zamani na hali hukuwa kitu).
(Maryam: 9).
   Alikuwa binaadamu kabla ya kuumbwa si chochote, ambae kamuweka na kumuumba ni Mwenyezi Mungu Mtukufu, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?). (Tuur: 35).

2:Na kuturuzuku: Tulipokuwa niwenye kuhitajia rizki chakula kinywaji mavazi nyumba vipando na mazuri, alitambua Mwenyezi Mungu Mtukufu shida zetu akawepesisha vilivyoko mbinguni na aridhini vyote kwa masilahi yetu kwaajili tubakie kwenye uhai, na kwaajili ya kuvitumia ili tufanye lengo la kuumbwa kwetu, nalo ni Ibada ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

3:Na hakutuacha bure: ni kitu kilicho achwa ambacho hakina faida yoyote, Mwenyezi Mungu ametuumba na kuturuzuku kwa hikma, hakutuumba kwa mchezo wala bure, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Je! Mlidhani ya kwamba tuli kuumbeni bure na yakwamba nyinyi kwetu hamtarejeshwa?). (Al-Muuminuun: 115).
Na akasema Mwenyez Mungu Mtukufu: (Ati anadhani mwanadamu kuwa ataachwa bure?* Kwani hakuwa yeye ni tone ya manii lilio shushwa?* Kisha akawa pande la damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo). (Al-Qiyamah: 36-38).
Na akasema: (Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utakao wapata). (Swaad: 27.(
Mwenyezi Mungu ametuumba na katuumbia hizi rizki na yanayo wezekana kwa hikma kubwa na lengo nzuri, nalo ni kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu, na wala hakutuumba kama wanyama ambao wameumbwa kwa maslahi ya viumbe kisha vinakufa na kuondoka; kwa sababu havija kalifishwa wala kuamrishwa wala kukatazwa, kwa hakika Ametuumba kwaajili ya ibada yake, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi* Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe* Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti). (Adh-Dhaariyaat: 56-58).
 
    Wala hakutuumba kwaajili ya maisha ya dunia tu, ili tuishi ndani yake, tukeshe tucheze, na tule na tunywe, tujitanue ndani yake kisha pisiwe na chochote, na kwa hakika maisha ni shamba, na sokoni ni nyumba ya akhera, tunajiandaa kwa matendo mema, kisha tunakufa na tunaelekea huko, kisha tunafufuliwa, kisha tuna hesabiwa na tunalipwa kwa matendo yetu.
Haya ndio makusudio ya kuumbwa majini na watu, na ushahidi wa hayo ni mwingi sana wakuonyesha kufufuliwa na malipo na hesabu, na akili inaonyesha hili, kwa sababu haiwezekani kwa hikma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuumba kiumbe waajabu, na akaufanya huu ulimwengu kwaajili ya binadamu kisha awaache wafe waondoke bila faida. Huu ni mchezo, hapana budi kujulikana majibu ya matendo katika nyumba ya akhera.
    Kwa hili kuna baadhi ya watu wanao maliza umri wao katika Ibada ya Mwenyezi Mungu na katika kumtii yeye, hali ya kuwa yupo katika ufakiri na shida, na huenda akawa ni mwenye kudhulumiwa kubanwa kuonewa na wala asilipiwe katika hii dunia, na kinyume chake, unakuta mwengine kafiri hamuamini Mungu na ni muovu lakini amekunjuliwa ana furaha katika hii dunia, ana neemeka amepewa anayo yataka, anafanya aliyo haramisha Mwenyezi Mungu, anawadhulumu waja anawafanyia vibaya, anakula mali zao, anaua bila haki, anawasaliti watu anajinyanyuwa kisha anakufa katika hali hiyo, hakupata chochote katika adhabu.
Je! Yafaa kwa uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na hekima zake amuache huyu mtiifu bila malipo?, na amuwache huyu kafiri bila kumlipa?, jambo hili halifai kutokana na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Kwa sababu hiyo kajaaliya nyumba ya akhera aliye fanya wema kulipwa kwa wema wake, na aliye fanya mabaya kwa mabaya yake, patadhihirika matunda ya matendo.
Dunia ni nyumba ya matendo, lakini akhera yao ni nyumba ya malipo, ima pepo au moto, na hakutuacha bure kama wanavyo dhani wasio muamini Mwenyezi Mungu na wanao amini uhai wa dunia bila akhera, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:  (Na walisema: Hapana isipokuwa huu uhai wetu wa duniani tunakufa na tunaishi, na hapana kinacho tuhiliki isipokuwa zama. Lakini wao hawana ilimu ya hayo, isipokuwa wao wanadhani tu). (Al-Jaathiyah: 24).
Haya ndio maneno ya wasio muamini Mwenyezi Mungu ambao hawaamini kufufuliwa.
Na kwa hakika Mwenyezi Mungu kawakanusha Akasema: (Kwani tutawafanya Waislamu mfano wa wakosefu?* Mna nini? Mnahukumu vipi?). (Al-Qalam: 35-36).
 
Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Je! Wanadhani wanao tenda maovu kuwa tutawafanya kama walio amini, na wakatenda mema, sawa sawa uhai wao na kufa kwao? Ni hukumu mbaya wanayo ihukumu!). (Al-Jaathiyah: 21).
   Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Ama! Tuwajaalie walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika ardhi? Au tuwajaalie wachamungu kama waovu?). (Swaad: 28).                                                                              Hili haliwezekani na wala haliwi.

BALI KATUTUMIA MITUME.
    Ilivyokuwa Ibada haifai tuichukue kutoka kwa Fulani na Fulani tutakao waona wazuri, au kumuiga Fulani na Fulani katika wanadamu, katutumia Mwenyezi Mungu Mitume watubainishie Namna tutakavyo muabudu; kwa sababu Ibada ni kitu rasmi, na haifai kumuabudu Mwenyezi Mungu kwa chochote isipokuwa kwa aliyo amrisha.
Ibada ni kitu rasmi juu ya yale walio kujanayo Mitume (s.a.w), na hekima ya kutumwa Mitume ili wawabainishie watu namna watakavyo muabudu Mungu wao, na wawakataze shirki na kumkufuru Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Hii ndiyo kazi ya Mitume (s.a.w), kwa sababu hii anasema Mtume (s.a.w): (Yeyote atakae zuwa katika dini yetu mambo ambayo hayapo atarejeshwa mwenyewe).
Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kabla ya hadithi (7350), na Muslim (18/1718), hadithi ya Bibi Aisha (r.a( .
Ibada ni kitu rasmi, na bida'a ni yenye kurejeshwa, na mambo yasio faa ni yenye kurejeshwa, na kufuata kama kipofu imekatazwa. Ibada hazichukuliwi isipokuwa katika sheria alio kujanayo Mtume (s.a.w).

BALI KATUTUMIA MTUME:
      Nae ni Muhammad (s.a.w) mwisho wa manabii, amemtuma ili atubainishie kwa nini Ametuumba? Na atubainishie namna ya kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu, na atukataze ushirikina na ukafiri na maasi, hii ndio kazi ya Mtume (s.a.w) na amefikisha kwa uwazi, na akatekeleza amana, na akaunasihi Umma (s.a.w), na akabainisha na akaweka wazi, na akatuacha katika njia nyeupe usiku wake ni kama mchana wake, yeyeto atakae kwenda kinyume ataangamia, kama ilivyo katika maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni Uislamu uwe ndiyo Dini).
(Al-Maaida: 3).

 

YEYOTE ATAKAE MTII ATAINGIA PEPONI, NA YEYOTE ATAKAE MUASI ATAINGIA MOTONI.
Atakae mtii, maana yake: kwa yale aliyo amrisha ataingia Peponi, na atakae muasi, maana yake: kwa yale aliyo kataza ataingia Motoni.
Ukweli wa haya ni mwingi ndani ya Qur-ani, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Mwenye kumti'i Mtume basi kwa hakika ndio amemti'i Mwenyezi Mungu). (An-Nisaa: 80).
 Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na mkimtii yeye mtaongoka). (An-Nuur: 54).
Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na mtiini Mtume, ili mpate kurehemewa). (An-Nuur: 56).
Yeyote atakae mtii ataongoka na ataingia Peponi, na yeyote atakae muasi atapotea na ataingia Motoni, amesema Mtume (s.a.w): (Nyoote mtaingia Peponi isipokuwa Yule atakaekataa, wakasema: ni nani atakae kataa ewe Mtume? Akasema: Yeyote atakae nitii Mimi ataingia Peponi na yeyote atakae niasi Mimi huyo ndiyo alie kata(.
Kapokea hadithi hii Imam Bukhari (7280). hadithi ya Abaa huraira (r.a).
Kauli yake Mtume (s.a.w): ATAKAE KATAA, maana yake: Amekataa kuingia Peponi. Na akasema Mtume (s.a.w): (Hato nisikia mimi yahudi au mkristo kisha hakuamini yale niliyo kujanayo isipokuwa ataingia Motoni).
Kapokea hadithi hii Imam Muslim (153), hadithi ya Abaa huraira (r.a).
      Yeyote atakae mtii ataingia peponi na yeyote atakae muasi ataingia motoni, na hii ndio tofauti kati ya muislamu na kafiri.
Na dalili kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni* Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamkamata mkamato wa mateso).  (Al-Muzammil: 15-16).  


Na dalili, maana yake: juu ya kutumwa Mitume kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni* Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamkamata mkamato wa mateso).
 Na maana ya: Tumemtuma: tumemtumia na tumemfunulia.
KWENU: Enyi makundi aina mbili majini na watu, ni maneno kwa watu wote; kwa sababu ujumbe wa Nabii Huyu unaenea watu wote hadi kusimama kiyama.
MTUME: ndie Muhammad (s.a.w).
SHAHIDI JUU YENU: maana yake: mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu siku ya kiyama kama yeye kakufikishieni ujumbe wa Mwenyezi Mungu na hoja ikasimama juu yenu, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Mitume hao ni wabashiriaji na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewa Mitume. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima).  (An-Nisaa: 165).
Asitokee yeyote siku ya kiyama akasema: mimi sijui kama nimeumbwa kwaajili ya Ibada, mimi sijui yepi ni lazima kwangu, na sijui yepi ni haramu kwangu, haiwezekani akasema haya, kwa sababu Mitume (s.a.w) wamekwisha wafikishia, na huu Umma wa Muhammad (s.a.w) utashuhudiya juu yao, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na vivyo hivyo tumekufanyeni muwe Umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume awe ni shahidi juu yenu).  (Al-Baqara: 143).
Umma huu utakuwa ni shahidi juu ya nyumati zilizo tanguliya siku ya kiyama kwamaba Mitume wao wamewafikishia ujumbe wa Mwenyezi Mungu, kwa yale walio yakuta ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa sababu Mwenyezi Mungu katusimulia habari za nyumati zilizo tanguliya na Mitume na walio yasema kwa nyumati zao.
Yote hayo tumeyajua kupitia kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu kitabu ambacho Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa na mwenye hikima, msifiwa.
NA ATAKUWA MTUME: Nae ni Muhammad (s.a.w), atakuwa ni shahidi juu yenu Ummati Muhammad, atashuhudia juu yenu mbele ya Mwenyezi Mungu kwamba yeye amesimamisha juu yenu hoja, na akafikisha kwenu Ujumbe, na akakupeni nasaha kwaajili Mwenyezi Mungu, hapatakuwa na hoja kwa yeyote siku ya kiyama kwa kusema: sikufikiwa na chochote, sikufikiwa na muonyaji, hadi makafiri Watakiri wakati watakapo tupwa motoni, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Kila mara likitupiwa kundi humo walinzi wake huwauliza: Kwani hakukujieni mwonyaji? Watasema: Kwani! Ametuijia mwonyaji, lakini tulimkadhibisha, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote. Nyinyi hamumo isipokuwa katika upotovu mkubwa!). (Al-Mulk: 8-9).
Wanasema kwa Mitume: Nyinyi mpo katika upotovu, wao wanawakadhibisha Mitume na kuwafanya ni wapotovu.
Hii ndio hikima ya kutumwa Mitume; kwaajili ya kusimamisha hoja kwa waja, na muongozo kwa yule anaetakiwa na Mwenyezi Mungu uongofu, Mwenyezi Mungu huwaongoza waja wake awatakao kupitia mitume, na husimamisha hoja juu ya wenye kupinga na kukanusha na kukufuru.
KAMA TULIVYO MTUMA MTUME KWA FIRAUNI: Mtume: ni Nabii Mussa (s.a.w), na Firauni ndie mfalme jeuri wa Misri, ambae alidai Uungu, na Firauni: ni jina la kubandikwa kila anae tawala Misri huitwa Firauni. Makusudio hapa ni Firauni alie dai Uungu: (Akasema: Mimi ndiye Mola wenu mkuu kabisa). (An-Naziat: 24).
LAKINI FIRAUNI ALIMUASI HUYO MTUME: Huyo ni Nabii Mussa (s.a.w), alipingwa na Firauni kama alivyo simulia Mwenyezi Mungu katika kitabu chake yaliyo tokea kati ya Nabii Mussa na Firauni, na alipo fikia Firauni na watu wake.
BASI TUKAMKAMATA,  Maana yake: Tulimkamata  Firauni kwa adhabu, nayo: hakika Mwenyezi Mungu alimzamisha yeye na watu wake ndani ya bahari kisha akawaingiza motoni: (Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni). (Nuuh: 25).
Akawa katika moto katika barzakhi (Kaburini), Amesema Mwenyezi Mungu  mtukufu:
)Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni). (Suuratul Ghaafir 46(.
Adhabu hii itakuwa kaburini kabla ya akhera,wataonyeshwa motoni asubuhi na jioni,yaani kuchomwa namoto mpaka kitakapo simama kiyama,na huu niushahidi tosha wakuthibitisha kuwepo kwa adhabu kaburini,Allah atukinge, Allah anasema:
(Na itapo fika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!) (Suuratul Ghaafir 46).

ADHABU TATU ZA WATU WA FIRAUN:
1-Hakika mwenyezi mungu aliwazamisha na kuwapoteza kwamuda mmoja.
2-Hakika wao wana adhibiwa Katika makaburi yao mpaka kitakapo simama kiyama.
3-Watakapo fufuliwa siku yakiyama wataingia katika adhabu kali,Allah atukinge.
Vilevile yeyote atakae muasi mtume (s.a.w) hakika mafikio yake yatakua katika adhabu kali kuliko Firauni, kwasababu mtume Muhamad (s.a.w) ni mtume bora kuliko mitume walio pita, atakae muasi adhabu yake inakuwa kubwa zaidi.
Mwenyezi mungu anasema kuhusu firauna: (basi tukamshika mshiko wa mateso).
Yaani kwa ukali na nguvu bila ulaini ndani yake.
Anasema Mwenyezi Mungu katika surati Hudi:{Na ndio kama hivyo ndivyo inavyo kuwa Mola wako Mlezi anapo ikamata miji inapo kuwa imedhulumu. Hakika mkamato wake ni mchungu na mkali.}
( Hudi 102).
Aya hii ni ushahidi tosha juu ya neema ya Mwenyezi mungu juu yetu kwa kumtuma mtume Muhamad (s.a.w) kwetu na hakika lengo la kumtuma ni kutubainishia njia sahihi ya kufanya ibada, yoyote atakae mtii ataingia peponi, na yoyote atakae muasi ataingia motoni, kama alivyo ingia firauni na watu wake motoni, pindi walipo muasi Nabii Mussa (a.s), vilevile maadui wa mitume wote hii ndio njia yao.
Mwenyezi Mungu mtukufu haridhii kushirikishwa nayoyote katika ibada.

MAS’ALA YA PILI:
Hakika Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yoyote katika ibada.
Haya mas’ala yanaambatana na mas’ala ya kwanza, kwa kuwa ya kwanza:
Yanabainisha uwajibu wa kumuabudu Mwenyezimungu na kumfuata mtume (s.a.w), na ndio maana ya shahada mbili, shahada ya (Lailaha ila Allah Muhamadu rasulu Allah).
Na mas’ala yapili: Nikwamba ibada inapo changanyika na ushirikina haikubaliwi, kwasababu ni lazima iwe ibada kwaajili ya Mwenyezi Mungu mshindi mtukufu.
Yoyote atakae muabudu Mwenyezi Mungu akamshirikisha na kitu kingine ibada yake inakuwa batili, kuwepo ibada hiyo na kuto kuwepo ni sawa, kwasababu ibada haifai bila ikhlas na kumpwekesha Mwenyezi Mungu, pindi zitakapo changanyika na ushirikina zitaharibika, kama alivyosema Mwenyezi Mungu mtukufu:{ Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako: Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye kukhasiri{.(Azzumar 65).
Na amesema Mwenyezi Mungu mtukufu:
}Na lau wangeli mshirikisha yangeli waharibikia waliyo kuwa wakiyatenda}(An'aam-88).
Ibada haiwezi kuitwa ibada ila ikiwa ni kwalengo la kumpwekesha Mwenyezi Mungu (tauhiidi), kama ilivyo swala haiwezi kuitwa swala mpaka uiswali ukiwa msafi (twahara(.
Ikichanganywa swala na kinacho tengua udhu basi kinaiharibu swala na kuibatilisha, ndio maana unakuta Mwenyezi Mungu anakusanya katika aya nyingi baina ya kuamrisha watu wafanye ibada na anawakataza shirki.
Alisema Mwenyezi Mungu:{Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote.{ (An-Nisaai-36).
Alisema Mwenyezi Mungu {Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti}. (Al-bayyinah 5).
Na alisema Mwenyezi Mungu:{Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu}. (Anbiyaa 25).
Mwenyezi Mungu kusema:{hapana mungu isipo kuwa Mimi}.
Kunamambo mawili:
1- kukanusha ushirikina.
2-kuthibitisha ibada kwa Mwenyezi Mungu mtukufu pekeyake.
Na alisema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu}. (Sura Al Israai23)
{Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani.} (An Nahl 36).
Amekutanisha baina ya kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na kujiepusha na ibada za matwaghuti (Mashetani).
Kwasababu ibada ya Mwenyezi Mungu haiwi ibada ila ikiwa ni pamoja na kujiepusha na matwaghuti, nao ni kufanya ushirikina.
Anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Basi anaye mkataa Shet'ani na akamuamini Mwenyezi Mungu bila ya shaka amekamata kishikio madhubuti, kisicho vunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.} (Al-Baqara256).
Kumuamini Mwenyezi Mungu peke yake haitoshi mpaka uyakufuru mashetani, na kama siyo hivyo hakika washirikina wanamuamini Mwenyezi Mungu pamoja na kuwa wanamshirikisha.
Anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:
{Na wengi katika wao hawamuamini Mwenyezi Mungu pasina kuwa ni washirikina}(yusuf 106).
Amebainisha Mwenyezi Mungu kwamba washirikina wanamuamini  Mwenyezi Mmungu, lakini imani yao wanaiharibu kwa kumshirikisha Mwenyezi Mmungu katika ibada zao.
Hii ndiyo maana ya kusema: yeyote mwenye kumuabudu Mwenyezi Mungu na akamtii Mtume (s.a.w) hakika mtu huyo hawezi kumshirikisha Mwenyezi Mmungu na chochote, kwasababu Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na chochote katika viumbe vyake.
Kutoka kwa abuu huraira (r.a) alisema: alisema Mtume (s.a.w) katika yale anayo yapokea kutoka kwa Mola wake mshindi mwenye nguvu: (Alisema Mwenyezi Mungu mtukufu: Mimi ndio tajiri wa washirika kwa ushirikina wanao ufanya, mwenye kufanya ibada yoyote akamshirikisha katika ibada hiyo asiyekuwa mimi basi nitamuacha na ushirikina wake). Amepokea hadithi hii imamu Muslim (2985).
Kuna watu wanaswali na wanashahidilia kuwa hapana Mola apasae kuabudiwa kwa kahi ila Mwenyezi Mungu, na Muhamad (s.a.w) ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na wanakithirisha kusema hivyo, na wanafunga na wanahiji, lakini wanayaomba makaburi, na wamuabudu Imamu Hassan na Husein, na Albadawiy, na Fulani na Fulani,
Na wanaomba nusura kwa watu walio kufa, hao ndio ibada zao nibatili, kwasababu wao wanamshirikisha Mwenyezi Mungu mshindi mwenye nguvu, wanachanganya ibada na ushirikina, basi ibada zao ni batili, na nizenye kuporomoka, mpaka watakapo mpwekesha Mwenyezi Mungu mshindi mwenye nguvu, na wamtakasie utii Mwenyezi Mungu na waache kuabudu kisichokuwa Mwenyezi Mmungu.
Na kama siyo hivyo hawatakuwa na chochote, basi ni wajibu kuzinduka kwa hilo, kwasababu Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na chochote katika ibada yake kwa vyovyote atakavyo kua.
Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yeyote atakavyo kua, ili asiseme yeyote: mimi nachukua kwa watu wema, na watu wazuri uombezi, mimi siabudu masanamu wala mizimu kama ilivyokua enzi za ujinga, mimi nawafanya hawa ni waombezi wangu na siwaabudu.
Tunamuambia kuwa: hayo ni maneno ya watu wa zama za ujinga waliwafanya waombezi wao kwa Mwenyezi Mungu kwasababu ni watu wema, na ni mawalii katika mawalii wa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu haridhii hayo.
Sio kwa malaika alie karibu na Mwenyezi Mungu wala Mtume aliye tumwa na Mwenyezi Mungu.
Malaika aliye karibu na Mwenyezi Mungu ni malaika bora, kama jibrilu amani ziwe juu yake, na malaika wanao ibeba arshi ya Mwenyezi Mungu, na malaika walio karibu nao, na malaika walio karibu na Mwenyezi Mungu mtukufu.
Pamoja na ukaribu na Mwenyezi Mungu na ukaribu wa waja wa Mwenyezi Mungu, na daraja kwa Mwenyezi Mungu, laiti angemshirikisha pamoja na asiye kuwa Mwenyezi Mungu pamoja na Mwenyezi Mungu katika ibada hakika Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa pamoja nae malaika alie karibu na Mwenyezi Mungu, wala Nabii aliye tumwa, kama Muhamad (s.a.w).
Na Nabii Issa na Nuhu na Ibrahim ambao ni Mitume walio pewa sheria, au walio tumwa kwa watu wote, au walio thibiti katika utume wao.
Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na yoyote, hata kama atakua ni mbora wa malaika, au ni mbora wa watu.
Yeye Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na yoyote katika malaika, au katika mitume, itakuaje kwa viumbe wasio kuwa mitume na malaika miongoni mwa watu wema na mawalii walio wema!
Basi wasio kuwa malaika na mitume ndio kabisa, hawezi Mwenyezi Mungu kumridhia kwa kumshirikisha pamoja nae kitu kingine, katika ibada.
Na haya ni majibu ya wale ambao wanao dai kwamba wao wanawafanya wale wema walio pita na mawalii uombezi kwa Mwenyezi Mungu ili awakurubishe hao kwa Mwenyezi Mungu, kama walivyo sema:{Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu} (Azzumar3).
Na kama siyo hivyo hakika wao wanaitakidi kwamba hao hawaumbi wala hawatoi rizki na hawamiliki kifo wala uhai wala kufufuka, bali makusudio yao ni kupata mtu wa katikati ili awaombee kwa Mwenyezi Mungu mshindi mwenye nguvu, kwasababu hiyo waliwafanyia ibada kwa lengo la kujikurubisha kwao, walichinja kwaajili ya makaburi, na wakatoa nadhiri kwa ajili ya ibada, na wakaomba nusra na kuwaita walio kufa.
Na ushahidi ni kauli ya Mwenyezi Mungu mtukufu:{Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu}
(Al-Jinn18(.
Mwenyezi Mungu haridhii kushirikiana na yeyote atakavyo kua, na haya yametajwa wazi katika Qur'an, na Sunna za Mtume Muhamad (s.a.w), lakini yeyote ambae hakuwa na akili wala mazingatio, na kuacha kufuaata mtu kipofu, na kuleta sababu ambazo ni batili, na azinduke na nafsi yake.
Na ushahidi kua Mwnyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yeyote, ni kauli ya Mwenyezi Mungu mtukufu: {Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu} (Al-Jinn18(
Misikiti ni nyumba za Mwenyezi Mungu, na ni sehemu zilizo andaliwa kwa ajili ya swala, nazo ni sehemu zinazo pendwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu, nazo ni nyumba ameidhinisha Mwenyezi Mungu zinyanyuliwe na litaje jina la Mwenyezi Mungu, na inapaswa iwe misikiti hii ni sehemu ya ibada ya Mwenyezi Mungu pekeyake, na kisitokee chochote katika misikiti ambacho ni cha kumshirikisha Mwenyezi Mungu, yasiwekwe ndani yake makaburi, kwasababu mtume (s.a.w) amemlaani mwenye kufanya kitendo hicho, na akaeleza kuwa kufanya hivyo ni kitendo cha mayahudi, na manaswara, na akatukataza kufanya hivyo mwisho wa uhai wake akiwa katika wakati wa kutolewa roho yake akisema: kutoka kwa Jundabi bin Abdillah albajaliy (r.a) alisema: alisema Mtume (s.a.w): "Fahamuni hakika walio kuwa kabla yenu walikua wakiyafanya makaburi ndio misikiti basi fahamuni msilifanye kaburi langu kua msikiti hakika mimi nawakataza hilo" Imepokelewa na Muslim (532(
alikuwa akiyasema haya akiwa katika wakati wa kutolewa roho yake.
Na kutoka kwa Aisha (r.a) alisema: alikuwa akisema Mtume (s.a.w) "Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya mayahudi na manaswara waliyafanya makaburi ya mitume wao kuwa ni misikiti" Ameipokea na Bukhari (435,436) na Muslim(531).
Misikiti inatakiwa itwaharishwe kutokana na athari za ushirikina na mizimu, na yasisimamiwe makaburi kwa kuyatukuza, au kuyajengea, bali misikiti ifanywe ni sehemu za ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, isimamishwe ndani yake swala, na litajwe jina la Mwenyezi Mungu ndani yake, na kisomwe ndani yake kitabu cha Mwenyezi Mungu, na ziwekwe ndani yake darsa mbalimbali zenye manufaa, na watu wakae itikafu kwaajili ya kufanya ibada, huu ndio wadhfa wa misikiti.
Ama kusimamishwa msikitini mizimu inayo abudiwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, basi hiyo sio misikiti, na kufanya hivyo ni ushirikina hata kama wenye misikiti hiyo wataiita kua ni misikiti, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema: {Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu…{.
Yaani misikiti siyo ya kisichokua Mwenyezi Mungu, na kwakuwa misikiti ni sehemu ya mkusanyiko wa watu, basi inatakiwa iwe ni sehemu twahara kutokana na ushirikina, na uzushi, na mambo yasiyo kubalika kisheria, kwasababu watu wanapata elimu na wanafanya ibada katika misikiti, pindi watakapo kuta katika misikiti ushirikina au mambo yasio faa kisheria huenda wakaathirika nayo au wakayachukua na kuyatangaza duniani kote, Kwahiyo ni wajibu iwe misikiti ni yenye kutwaharishwa kutokana na ushirikina.
Na miongoni mwa misikiti mitukufu kulio yote ni msikiti mtukufu wa Makkah, kama alivyo amrisha Mwenyezi Mungu alie tukuka alie wa juu utwaharishwe, alisema Mwenyezi Mungu mtukufu:
}Na pale tulipo muweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia: Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu, na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao sujudu} (Hajj 26(.
Mwenyezi Mungu aliutwaharisha kutokana na nini? aliutwaharisha kutokana na ushirikina na uzushi na mambo yasiyo kubalika katika dini kama alivyo utwaharisha kutokana na na najsi au uchafu wa takataka.
Msiombe enyi watu pamoja na Mwenyezi Mungu yeyote, msiombe nusra kwa yoyote pamoja na Mwenyezi Mungu, kama vile kusema: ewe Mwenyezi Mungu, ewe Muhammad, ewe Mwenyezi Mungu, ewe Abdul Qaadir,

au kusema: ewe Abdul Qaadir, ewe Muhamad, au mfano wa hayo, hakika Mwenyezi Mungu haridhii hayo na hayakubali.
Hakuna yeyote anae toka katika hukumu hiyo hakuna malaika alie karibu na Mwenyezi Mungu, wala mtume alie tumwa na Mwenyezi Mungu, wala sanamu au mzimu, wala kaburi la shekh, au walii, wala aliye kufa, vyovyote atakavyo kuwa.
Qauli ya Mwenyezi Mungu {…basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu} (Al-Jinn18).
Inakusanya wote wenye kuombwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, na Aya hii imeonyesha kuwa ibada  haikupi manufaa mpaka uifanye ukiwa na Tauhiidi, na kwa hakika ukiichanganya na ushirikina basi inabatilika, na inakua ni mzigo kwa mfanyaji, kisha akasema Mwenyezi Mungu: {Nahakika misikiti ninyumba za Mwenyezi Mungu...} ni wajibu ijengwe misikiti kwa nia ilio takasika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na siyo kwa ajili ya kujionyesha, au kutaka asikike, au kwasababu ubaki utajo wake baada ya kufa kama wanavyo sema, au uwe msikiti ni athari za kiislam, kujenga msikiti kwa sababu ya mambo hayo haifai.
Misikiti inajengwa kwasababu ya kufanya ibada, na kwa nia ya kufanya ibada, na iwe nia imetakasika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mwenye nguvu alie tukuka, na misikiti inajengwa kwa lengo la kuchuma thawabu, na haijengwi kwasababu ya kuchuma haramu, kwasababu misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, Kutoka kwa Abii Hurayra (r.a) alisema: alisema Mtume (s.a.w): "Na hakika Mwenyezi Mungu hapokei ila kitu kizuri" Imepokelewa na Muslim (1015).
Na misikiti inajengwa kwa pesa ya halali, na iwe niya ya kujenga hiyo misikiti ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mwenye nguvu aliye tukuka, hataki ingwe kwa sifa za watu au kubakia utajo wa mtu, au kujionyesha au kutaka asikike, hakika kujenga msikiti ni ibada na ibada ni wajibu iwe kwaajili ya Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu.  
Ndugu katika imani hii nisehemu ya pili katika kitabu hiki cha Masomo katika umuhimu wa Tawhiid .(2) Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah cha Imamu Fawzani Allah amuhifadhi tuwe pamoja katika sehemu ya tatu Allah akiipenda .
Wabillah Tawfiiq.